Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya jiji la Mwanza Bi Eluminata Mwita akisikiliza jambo kwa makini toka kwa wajumbe (hawapo pichani). |
Halmashauri pamoja
na wadau toka mashirika na taasisi za kutetea na kulinda haki za watoto jijini
Mwanza wameanza rasmi vikao vya maandalizi ya kuadhimisha sherehe za siku ya
mtoto wa Afrika inayoadhimishwa kila Mwaka Juni 16.
Kikao hicho kilichofanyika
katika ukumbi wa Halmashauri wa Jiji la Mwanza chini ya Afisa Maendeleo ya Jamii
wa Halmashauri hiyo Bi. Eluminatha Mwita wajumbe walikubaliana kuadhimisha siku
hiyo katika Kata ya Buhongwa, kwa Wilaya ya Nyamagana.
Siku ya mtoto wa
Afrika huadhimishwa kimataifa kote duniani kwa lengo la kutambua thamani, utu,
na umuhimu wa mtoto duniani. Maadhimisho haya hufanywa kila juni 16 tangu ilipotangazwa
kuwa siku rasmi mwaka 1991 na jumuiya ya umoja wa Afrika.
Akizungumza wakati
wa kufungua kikao hicho Afisa Maendeleo Jamii wa Jiji la Mwanza Bi. Eluminatha
Mwita alisema kuwa kauli Mbiu ya mwaka huu ni “Kuondoa Mila Zenye Kuleta Madhara kwa Watoto ni Jukumu Letu Sote”
na kufafanua kuwa kauli hiyo inalenga kuwasisitiza wazazi na walezi kuacha mila
potofu zenye kuleta madhara kwa watoto.
Bi Eluminatha
alisema kuwa “Kauli mbiu hiyo ina lenga kuangalia mila zote kandamizi na potofu
zinazotokana na jamii husika katika malezi ya mtoto na kusababisha madhara
mbalimbali ikiwemo kuongezeka kwa watoto wa mitaani, kubakwa kwa watoto, kukosa
elimu, afya na malezi bora pamoja na vifo kwa watoto hawa”.
Kikao hicho cha
kwanza kiliweza kuchagua viongozi wa kamati hiyo ya maandalizi, mwenyekiti aliyechaguliwa
ni Godfrey Salum huku katibu ni Devis Mrope na katibu msaidizi akichaguliwa
Francisca Michael, baada ya kupata viongozi kamati nne ziliundwa na wajumbe,
Kamati ya Uratibu, Mipango na Fedha, Kamati ya Usafiri na Ulinzi, Kamati ya
Mapambo na Burudani pamoja na kamati ya Hotuba na Habari.
Imeandaliwa
na Afisa Habari wa Kamati ya Maandalizi
Maadhimisho
ya Siku ya Mtoto wa Afrika - Mwanza
Hassan
Mrope
0713441892
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni