Alhamisi, 17 Aprili 2014

TOKA BBC SWAHILI: MSICHANA ALIYETESWA KINYAMA KWA MIAKA 9


Polisi nchini Argentina wamemwokoa msichana mwenye umri wa miaka kumi na mitano ambaye alifungiwa katika chumba cha kuegesha magari na kunyimwa chakula pamoja na kupigwa na wazazi waliokuwa wamemuasili, kwa kipindi cha miaka tisa.
Msichana huyo alikuwa na uzani wa kilo ishirini pekee.

Amesema alifanikiwa kuondoka katika eneo hilo la kuegesha magari mara mbili tu katika kipindi cha miaka tisa.Viumbe wa pekee walioishi naye ni mbwa pamoja na Tumbili. Msichana huyo amesema alipigwa kila mara iwapo angejaribu kula mabaki ya chakula kilichotupwa kwa wanyama hao.

Walezi wake wamekamatwa na kufunguliwa mashItaka ya kumdhulumu na kumweka kama mtumwa msichana huyo.
Msichana huyo ambaye amelazwa hospitlaini, alipatikana na dadake wa kuzaliwa naye mjini Buenos Aires.
Kwa mujibu wa maafisa wakuu, wazazi hao walimuasili mwaka 2001 baada ya mahakama kuamua kuwa wazazi wake wa kumzaa hawakuwa na uwezo wa kifedha kuweza kumlea.
Walikuwa wanasubiri stakabadhi za kukamilisha mpango wa kumuasili mtoto huyo.

KUTOKA BBC SWAHILI: JELA KWA KUMKATA KICHWA MPENZI WAKE.

Mwanamume aliyemuua kwa kumkata kichwa mpenzi wake amepatikana na hatia ya mauaji nchini Uingereza
Aras Hussein alimkata kichwa mwanafunzi mwenye umri wa miaka 18 Reema Ramzan nyumbani kwake katika mtaa wa Sheffield mwezi Juni kabla ya yeye mwenyewe kujidunga kisu kifuani mwake.

Hussein, alikiri kumuua mpenzi wake baada ya kuzozana ingawa awali alikana madai ya mauaji.Aras amehukumiwa kifungo cha maisha jela. Mwili wa Ramzan ulipatikana katika sehemu ya jikoni ya nyumba ya Hussein tarehe nne mwezi Juni.

Polisi walipigiwa simu na mpita njia mmoja aliyemuona Hussein akitembea uchi nje akiwa na damu katika mwili wake. Madaktari walipojaribu kumsaidia kwa kumpa huduma ya dharura aliwauliza kwa nini walikuwa wanataka kumsaidia wakati amemuua mtu nyumbani kwake.
Alipoulizwa kwa nini alifanya hivyo, akajibu kuwa hajui. Mahakama ilisikia ambavyo msichana huyo alidungwa kisu kifuani na kisha kukatwa kichwa chake. Pia mikono yake ilikuwa na alama za kuonyesha kuwa alijaribu kujikinga kutokana na kushambuliwa na mpenzi wake
Kiongozi wa mashitaka aliambia mahakama kuwa marehemu Ramzan bado alikuwa hai wakati Aras alipoanza kumkata koo kwa kutumia nguvu. Wakati kesi ilipokuwa inaendelea , mahakama iliambiwa na familia ya Ramzan kuwa hawakupenda uhusiano kati ya wawili hao. Siku ya kuuliwa kwake, alikuwa amekwenda nyumbani kwa Aras akiwa na Pasi yake ya usafiri pamoja na kitita kikubwa cha pesa.

Jumanne, 15 Aprili 2014

TAASISI YA KIVULINI YAANZA VIKAO VYA TATHMINI YA UTENDAJI KAZI KWA WASAIDIZI WA KISHERIA KATIKA WILAYA ZA SENGEREMA, MAGU, MISUNGWI NA KWIMBA MKOANI MWANZA.

Mkurugenzi wa Shirika la KIVULINI Bw. Ramadhan Masele akizungumza na Wasaidizi wa Kisheria (hawapo pichani) wilaya ya Sengerema cha tathmini ya utendaji kazi wa Wasaidizi wa kisheria chini ya mradi wa msaada wa kisheria na haki za binaadamu kilichoanza mapema asubuhi.

Baadhi ya wasaidizi wa kisheria katika wilaya ya Sengerema wakiwa katika kikao cha tathmini ya utendaji kazi wao kwa kipindi cha robo ya pili ya Mwaka kwa mradi wa  mradi wa msaada wa kisheria na haki za binaadamu.
Bi Eunice Mayengela Mwanasheria toka Shirika la KIVULINI akitoa ripoti ya utendaji kazi wa Mradi wa msaada wa kisheria na haki za binaadamu kwa washiriki. Bi. Eunice alisema kuwa Lengo la umoja wa Wasaidizi wa kisheria ni kuhakikisha unasimamia shuguli zote za msaada wa kisheria katika wilaya husika, na ni kiunganishi cha wasidizi wa kisheria katika ngazi ya wilaya.
Bi Eunice Mayongela akisisitiza jambo kuhusu Mkutao wa siku moja ulifanyika katika wilaya ya sengerema  kwa lengo la kuzungumzia maendeleo ya mradi  na changamoto zinaojitokeza.

Mkurugenzi wa Shirika la KIVULINI akisisitiza Katika kipindi hiki Kivulini iliweza kutengeneza vitabu kwa ajili ya kuandikishia shauri, kutolea rufaa ,na kupata mrejesho wa rufaa kutoka kwa watoa huduma wengine na kugawanywa kwa wasidizi wa kisheria, Pia Kivulini iliweza kuwatengenezea vitambulisho wasidizi wa kisheria ili waweze kutambulikana kwa urahisi Zaidi katika jamii zao.

Baadhi ya Wasaidizi wa Kisheria toka wilaya ya Sengerema wakisikiliza kwa makini ripoti ya kiutendaji katika wilaya ya Sengerema, Mwanza.
Sengerema, Mwanza.

Taasisi isiyo ya kiserikali inayojishughulisha na kutetea haki za Wanawake, KIVULINI, yenye makao makuu jijini Mwanza imeanza kufanya vikao vya tathmini ya utendeji kazi wa wasaidizi wa kisheria kwa robo mwaka ya pili katika ngazi za wilaya chini ya mradi wa msaada wa kisheria na haki za binaadamu.

Vikao hivyo vilivyoanza leo katika wilaya ya Sengerema kwa kukutana na wasaidizi wa kisheria 25 wanaofanya kazi ya kutatua migogoro ya kisheria katika vijiniwilaya ya sengerema huku vikao hovyo vinatarajiwa kufanyika pia katika wilaya ya Magu, Misungwi na Kwimba zote zipo ndani ya mkoa wa Mwanza.

Kivulini kupitia mradi wa msaada wa kisheria imetekeleza shughuli mbalimbali kwa lengo la kuisaidia jamii kupata uelewa wa haki zao za kisheria na pia kundeleza uwepo wa elimu na ushauri wa kisheria katika maeneo ambayo mradi unatekelezwa.

Na juhudi kubwa imewekwa katika kuwajengea uwezo wasaidizi wa kisheria kwasabaabu wasidizi wa kisheria wanaitajika ili kuiwezesha jamii kuweza kupata haki hasa wale walioko pembezoni.Na kwa kupitia umoja wa wasaidizi wa kisheria wataweza kutoa elimu kwa wanajamii ili waweze kujua haki zo za kisheria .na matatizo yanayopelekea uvunjifu wa haki na kuchukua hatua.

Kivulini Iliwezesha uundwaji wa umoja wa vikundi vinne vya  wasaidizi wa kisheria ktika wilaya ya kwimba,Misungwi,Sengerema,Na Magu  na umoja huo unaundwa na jumla ya wajumbe 25 kila kikundi ambao walipata mafunzo ya wasaidizi wa kisheria kwa kutumia mtaala wa chama cha wanasheria Tanganyika.

Wasaidizi wa kisheria wameendelea kutoa huduma ya ushauri wa kisheria kwa wanajamii  hasa kwa makundi yasiyojiweza katika kata 52, kwa kipindi cha robo mwaka ya pili wasaidizi wa kisheria wamepokea mashauri 129 kwa ujumla katika mashauri hayo yaliyokamilika ni mashauri 60 yaliyotolewa rufaa ni 43 na yanayoendelea nimashauri 43, ukilinganisha na robo mwaka ya kwanza ambapo mashauri 200 yalipokelewa ambayo inafanya jumla ya mashauri 329 yaliyopokelewa na wasaidizi wa kisheria.

Ijumaa, 11 Aprili 2014

KONGAMANO LA KIPEKEE KWA MABINTI WA VYUO VIKUU DODOMA


HUDUMA ZA DHARURA KWA WAZAZI KIBITI ZAOKOA MAISHA YA MAMA NA MTOTO

Mmoja wa akinamama aliyepatiwa huduma za uzazi katika Kituo cha Afya Kibiti kinachotoa huduma za dharura kwa akinamama wajawazito akizungumzia msaada wa huduma hiyo kwa wajawazito
Baadhi ya akinamama wakipatiwa huduma katika kituo cha afya Kibiti leo.
Mratibu wa Mtandao wa Utepe Mweupe Kitaifa (The White Ribbon Alliance), Rose Mlay akimjulia hali mmoja wa akinamama aliyejifungua katika wodi ya wazazi katika Kituo cha Afya Kibiti leo.
Mratibu wa Mtandao wa Utepe Mweupe Kitaifa (The White Ribbon Alliance), Rose Mlay akitambulishwa kwa baadhi ya wahudumu katika wodi ya wazazi kwenye Kituo cha Afya Kibiti leo alipotembelea kuangalia mwenendo wa utoaji huduma za dharura katika kituo hicho.

********************************

MGANGA Mfawidhi wa Kituo cha Afya Kibiti, Chagi Jonas Lymo amesema uwepo wa huduma za dharura kwa wajawazito katika kituo hicho cha afya umesaidia kiasi kikubwa katika uokoaji wa maisha ya mamamjamzito pamoja na vifo vya watoto eneo hilo.

Lymo ametoa kauli hiyo leo mjini Kibiti alipokuwa akizungumza na Mratibu wa Mtandao wa Utepe Mweupe Kitaifa (The White Ribbon Alliance), Rose Mlay pamoja na Mkurugenzi wa World Lung Foundation walipotembelea kituo hicho kuangalia namna kinavyotoa huduma kwa wananchi na changamoto zake.

Akizungumza zaidi, Lymo alisema tangu Kituo cha Afya cha Kibiti kuanza kutoa huduma za dharura kimekuwa msaada mkubwa kwa akinamama wajawazito eneo hilo na kwa sasa idadi ya akinamama wanaojifungulia eneo hilo imeongezeka mara tatu zaidi tofauti na ilivyo kuwa awali jambo ambalo unaonesha wamevutiwa na huduma hiyo muhimu kwa wajawazito.

Alisema kwa sasa kituo hicho kinafanya upasuaji kwa matatizo yote ya uzazi kwa wajawazito, ikiwemo kutoa huduma za kuongezewa damu kwa wajawazito wenye mahitaji jambo ambalo limesaidia kwa kiasi kikubwa kuokoa maisha ya mama mjamzito pamoja na mtoto mtarajiwa.

"...Awali tulikuwa hatutoi huduma za upasuaji kwa akinamama wajawazito...tulikuwa hatuna chumba cha upasuaji hivyo tulitoa huduma za uzazi za kawaida, na ilipotokea matatizo kwa mjamzito tulimshauri kwenda ama kwenye hospitali ya Mchukwi (ya kulipia) ambayo ipo umbali wa takribani kilometa 15 au kwenda kwenye Hospitali ya Wilaya Utete ambayo ni kilometa 84 kutoka hapa," alisema.

"...Baada ya kuanzisha huduma za upasuaji kwa akinamama wajawazito, akinamama waliokuja kujifungulia hapa waliongezeka..., mwezi wa kwanza tu wa kuanza kutoa huduma hizi wakinamama waliongezeka kutoka idadi ya wagonjwa 35 kwa mwezi waliongezeka hadi kufikia zaidi ya akinamama 100 kwa mwezi," alisema Lymo.

Alisema kwa mwezi uliopita (Machi) jumla ya wajawazito 135 walifika kupata huduma za uzazi kiasi ambacho kwa sasa ni kikubwa na kinazidi uwezo wa kituo, jambo ambalo alishauri ipo haja ya kituo hicho kuongezewa mahitaji anuai ili kwenda sambamba na ongezeko la wateja wake kwa sasa.

Kwa upande wake Mratibu wa Mtandao wa Utepe Mweupe nchini, Bi. Rose Mlay alisema serikali ikiamua kwa kushirikiana na wadau wengine inaweza kumaliza matatizo ya vifo kwa wajawazito pamoja na watoto kwa kusogeza huduma za dharura katika vituo vya afya ambavyo vingi vipo karibu na wananchi.

"...Inawezekana kabisa kupambana na vifo vya akinamama wajawazito pamoja na watoto endapo Serikali ikijipanga na kuamua vituo vya afya viwekewe bajeti ya kutosha na hatimaye kuweza kutoa huduma za dharura kwa akinamama wajawazito na watoto," alisema Bi. Mlay.

World Lung Foundation ndiyo taasisi iliyokiwezesha kituo cha Afya cha Kibiti kuweza kutoa huduma za dharura kwa akinamama wajawazito. Akizungumzia hatua hiyo, Mkurugenzi wa World Lung Foundation, Dk. Nguke Mwakatundu alisema taasisi hiyo imevisaidia jumla ya vituo 10 vya afya kutoa huduma za dharura pamoja na kuziwezesha hospitali nyingine tano katika nyanja tofauti kwenye utoaji huduma za afya.

Jumatano, 9 Aprili 2014

MILA NA TAMADUNI POTOFU ZAZIDI KUWAKANDAMIZA WANAWAKE NCHINI, JAMAA AAMUA KWENDA KUMUOA MAMA YAKE KAMA URITHI BAADA YA BABA YAKE MZAZI KUFARIKI

Mila na tamaduni potofu za baadhi ya jamii za Kiafrika na Tanzania ikiwemo zimekuwa zikitajwa kuendelea kuwa kandamizi kwa binadamu hasa wa jinsi ya kike ambapo vitendo mbalimbali vya unyanyasaji vimekuwa vikiripotiwa kutokea kwa jamii hizo ambapowatu wenye  jinsi ya kike wamekuwa wahanga wakubwa wa mila na desturi hizo.

Yafuatayo ni mahujiano yaliyofanywa na Clouds Fm ya jijini Dar ambapo imeripoti kuwa Mama mmoja mkazi wa Kimara jijini Dar es salaam amekimbiwa na Mumewe aliyeenda kwao kuoa kwa kumrithi mke wa marehemu baba yake mzazi baada ya baba yake huyo kufariki. 

Ebu sikiliza kisa hiki kupitia kipindi cha Heka Heka cha Clouds Fm kisha tupe maoni yako.

ZAWADI YA KUFELISHA

Mratibu wa Elimu Kata Mursagamba wilayani Ngara mkoani Kagera, George Rwetabura akipokea Kinyago kutoka kwa Katibu Tawala, Vedastus Tibaijuka baada ya kata yake kuwa ya mwisho kitaaluma kati ya kata 20 za wilaya hiyo. Picha na Shaaban Ndyamukama, Mwananchi.