![]() |
Mwanafunzi wa kike akidanganywa jambo na mtoto wa kiume, hali hii huchangia zaidi kupotea kwa ndoto za wanafunzi wa kike. Picha na na habari: Mwananchi |
Picha
hii inatoa ushuhuda wa vikwazo wanavyokumbana navyo wanafunzi wa kike wakiwa
njiani kwenda au kurudi shule.
Mwandishi
wetu alimwona mwanafunzi huyu akizongwa na kijana huyu mkware katika eneo la
makaburi ya Bahi Road mkoani Dodoma.
Japo
wahusika walionekana kujuana, msichana huyu anayesoma Shule ya Sekondari Kikuyu
iliyopo Manispaa ya Dodoma, alikiri kuwa maongezi yao yalikuwa yakielekea
kubaya kiasi cha kuamua kukimbia.
Kadhia
hii ilimkumba msichana huyu akiwa njiani. Anapoishi na ilipo shule kuna umbali
wa karibu kilomita tano.
Vikwazo kwa watoto wa kike
Pamoja
na mikakati iliyopo ya kuwasaidia watoto wa kike kupata elimu, hali halisi
katika maeneo mengi nchini inaonyesha kuwa bado kuna vikwazo mbalimbali
vinavyowazuia wasichana kupata haki hiyo ya msingi.
Kwa
mfano, mara kwa mara wadau wa elimu kupitia ripoti zao wamekuwa wakisema watoto
wa kike nchini wakiwamo wanafunzi hawako salama.
Wanafunzi
hao ni waathirika wakubwa wa vitendo mbalimbali vya unyanyasaji wa kijinsia
ikiwamo kubakwa. Ukweli ni kwamba wanafunzi wa kike hawako salama nyumbani,
njiani wanapoelekea au kurudi shule na hata shuleni kwenyewe.
Unyanyasaji
njiani ni kwa sababu shule nyingi hasa zilizo maeneo ya vijijini, ziko mbali na
makazi ya watu, hivyo wasichana wanalazimika kutembea masafa marefu.
Umbali
huu una athari kwa watoto wa kike, kama vile kuchokozwa na wahuni, kurubuniwa
na wanaume wakware na hata kubakwa.
Katika
baadhi ya maeneo, wanafunzi hao wanalazimika kupita katika maeneo hatarishi
kama vile porini. Tukio la mwanafunzi huyu ni ushahidi kuwa wasichana hawako
salama. Hata baadhi ya matukio ya ujauzito shuleni huanza kwa namna hii.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni